Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Azam wamkabidhi rungu rasmi Moallin
Michezo

Azam wamkabidhi rungu rasmi Moallin

Spread the love

 

KLABU ya Azam Fc inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara imemtangaza Abdihamid Moallin kuwa kocha mkuu wa kikosi hiko kwa mkataba wa miaka mitatu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Moallin alisaini mkataba huo hii leo jijini Dar es Salaam, tarehe 25 Januari 2022, mbele ya mtendaji Mkuu wa timu hiyo Abdukarim Amin (Popat).

Kocha huyo ambaye hapo awali, alirithi mikoba ya George Lwandamina, aliyetimuliwa kwenye klabu hiyo kufuatia matoke mabovu.

Mara baada ya kusaini mkataba huo, Moallin alisema kuwa anaamini uwezo wa klabu ya Azam Fc, na anaimani itafika mbali, kutokana na ukubwa walionao.

“Azam FC ni klabu kubwa, na nililiona hili siku ya kwanza tu nilipofika hapa, nina amini katika klabu hii, nina amini katika uwezo wa klabu hii, klabu hii ina nafasi ya kufanya makubwa,”- Abdihamid Moallin, Kocha Mkuu Azam FC

Kocha huyo hapo awali alikuja ndani ya Azam Fc, kushika nafasi ya Mkurugenzi wa Ufundi wa Maendeleo ya Soka la Vijana, lakini alijikuta kwenye majukumu ya ukocha wa timu ya wakubwa kwa muda na kufanya vizuri kwenye michezo yake.

Toka alikabidhiwa kikosi hiko mwishoni mwa mwaka jana, Moallin alionesha uwezo mkubwa kwa kuleta mabadiliko kwenye kikosi cha klabu hiyo, huku akifika Fainali ya Kombe la Mapinduzi, na kupoteza dhidi ya Simba SC.

Katika michezo ya Ligi kuu Tanzania Bara kocha huyo amepoteza mchezo mmoja tu, dhidi ya Simba kwa mabao 2-1, uliopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!