Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kuanzia Zanzibar, Tamasha wiki ya Mwananchi
Michezo

Yanga kuanzia Zanzibar, Tamasha wiki ya Mwananchi

Spread the love

 

Klabu ya soka ya Yanga itazindua rasmi wiki ya Mwananchi visiwani Zanzibar Agost 22, mwaka huu, kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii, kuelekea kilele cha Tamasha la siku ya mwananchi. Anaripoti Wiston Josia TUDARCo…(endelea)

Tamasha hilo litafanyika Agosti 29, 2021 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Afisa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa uzinduzi wa wiki hiyo utafanyika Zanzibar na kuwataka mashabiki wa klabu hiyo kujiandaa kurudisha kwa jamii.

“Uzinduzi utafanyika Zanzibar Agosti 22, na mtaona nini kitakwenda kutokea, wanayanga wajiandae kwa kurudisha kwa jamii kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii.” Alisema Afisa Habari huyo

Yanga watakwenda kufanya tamasha hili kwa mara ya tatu mfululizo, huku likitumika kama jukwaa la kuwatambulisha wachezaji wapya waliosajiliwa na klabu hiyo kwa msimu huu.

Aidha Bumbuli aliendelea kusema kuwa wao kama Yanga na kwa kushirikiana na wadhamini wao kampuni ya GSM, wamechangia kiasi cha shilingi 50 milioni kusaidia uwendeshaji wa Ligi visiwani Zanzibar katika hafla maalumu iliyoudhuliwa na makamu wa pili wa Rais visiwani humo Hemed Suleiman Abdulla.

“Yanga na GSM tumechangia Shilingi 50 milioni kusaidia uwendeshaji wa Ligi ya Zanzibar mbele ya makamu wa pili wa Rais.” Alinena Bumbuli

Hassan Bumbuli, Afisa Habari wa Yanga

Katika hatua nyingine Afisa Habari huyo alizungumzia kuhusu maendeleo ya kambi ya timu hiyo nchini Morocco ambapo alisema kuwa, wachezaji wameshaanza mazoezi na suala la usajili limeshakamilika pamoja na kupata vibari vya uhamisho wao (ITC)

“Wachezaji wameshaanza mazoezi, na kuhusu usajili tumekamilisha usajili wa kimataifa na ITC zote zimekamilika isipokuwa ya Kharid Haucho ambaye klabu yake ilkuwa bado haijatoa ila ndani ya siku mbili yatakamilika.” Alifunguka kiongozi huyo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!