Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri azuia wananchi kumpongeza Rais Magufuli
Habari za Siasa

Waziri azuia wananchi kumpongeza Rais Magufuli

Spread the love

LUHAGA Mpina Waziri wa Mifugo na Uvuvi,  amepiga marufuku makongamano ya wafugaji ya kumpongeza Rais John Magufuli,  kwa muda mpaka pale kazi waliyopewa kama Tume itakapokamilika. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na Wananchi wa Kisesa mkoani Mwanza amesema kuwa huu siyo muda wa kuandamana na badala yake watumie muda  huo kuisaidia tume iliyondwa na Rais kwa ajili ya kusuluhisha migogoro ya ardhi kwenye jamii ya wafugaji na wakulima.

Rais Magufuli ameunda tume maalumu ya uchunguzi ya usuluhishi wa migogoro ya ardhi kwenye jamii za wafugaji na wakulima.

Baadhi ya mawaziri kwenye tume hiyo ni pamoja Mpina, William Lukuvi, Waziri wa Ardhi  na Dk. Hussein Mwinyi,mn Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Mpina amesema tume nyingi zilizoundwa miaka ya nyuma kushughulikia migogoro hiyo zilichakachuliwa hata kabla ya kukabidhi matokeo ya mambo waliyobaini kwa kuwa kwenye migogoro hiyo wako baadhi ya viongozi wa Serikali wako nyuma wana manufaa binafsi wanayopata ndio maana mapendekezo yaliyotolewa ya kutatua migogoro hiyo hayajawahi kutekelezwa hadi leo.

Amesema baadhi ya watendaji wa serikali walilazimika hata kutoa rushwa ili kubadilisha maamuzi ya tume zilizokuwa zinaundwa kushughulikia migogoro hiyo kwa sababu wananufaika na migogoro hiyo.

“John Pombe Magufuli akasema hapana nitaunda tume ambayo haitapokea rushwa timu ya Lukuvi mnaiona ina sura ya kupokea rushwa?

“Vichwa vya kina Mpina unaweza ukawapa nini wakakubali, akasema wananchi wangu watahangaika mpaka lini, watauana mpaka lini mifugo mingi imedhulumiwa kwa kivuli cha uhifadhi, Rais akasema nitaunda tume ndio hii sasa ya mawaziri,” alisema Mpina.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!