Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri azuia wananchi kumpongeza Rais Magufuli
Habari za Siasa

Waziri azuia wananchi kumpongeza Rais Magufuli

Spread the love

LUHAGA Mpina Waziri wa Mifugo na Uvuvi,  amepiga marufuku makongamano ya wafugaji ya kumpongeza Rais John Magufuli,  kwa muda mpaka pale kazi waliyopewa kama Tume itakapokamilika. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na Wananchi wa Kisesa mkoani Mwanza amesema kuwa huu siyo muda wa kuandamana na badala yake watumie muda  huo kuisaidia tume iliyondwa na Rais kwa ajili ya kusuluhisha migogoro ya ardhi kwenye jamii ya wafugaji na wakulima.

Rais Magufuli ameunda tume maalumu ya uchunguzi ya usuluhishi wa migogoro ya ardhi kwenye jamii za wafugaji na wakulima.

Baadhi ya mawaziri kwenye tume hiyo ni pamoja Mpina, William Lukuvi, Waziri wa Ardhi  na Dk. Hussein Mwinyi,mn Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Mpina amesema tume nyingi zilizoundwa miaka ya nyuma kushughulikia migogoro hiyo zilichakachuliwa hata kabla ya kukabidhi matokeo ya mambo waliyobaini kwa kuwa kwenye migogoro hiyo wako baadhi ya viongozi wa Serikali wako nyuma wana manufaa binafsi wanayopata ndio maana mapendekezo yaliyotolewa ya kutatua migogoro hiyo hayajawahi kutekelezwa hadi leo.

Amesema baadhi ya watendaji wa serikali walilazimika hata kutoa rushwa ili kubadilisha maamuzi ya tume zilizokuwa zinaundwa kushughulikia migogoro hiyo kwa sababu wananufaika na migogoro hiyo.

“John Pombe Magufuli akasema hapana nitaunda tume ambayo haitapokea rushwa timu ya Lukuvi mnaiona ina sura ya kupokea rushwa?

“Vichwa vya kina Mpina unaweza ukawapa nini wakakubali, akasema wananchi wangu watahangaika mpaka lini, watauana mpaka lini mifugo mingi imedhulumiwa kwa kivuli cha uhifadhi, Rais akasema nitaunda tume ndio hii sasa ya mawaziri,” alisema Mpina.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!