Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watoto walioweka rekodi GGML KiliChallenge, wang’ara siku ya mashujaa
Habari Mchanganyiko

Watoto walioweka rekodi GGML KiliChallenge, wang’ara siku ya mashujaa

Spread the love

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama amewapongesa watoto Abel Mussa na Rebbeca Damian wenye umri wa miaka 14 waliopanda mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya GGML KiliChallenge- 2023, huku watoto hao wakibainisha kuwa hatua yao hiyo ililennga kuunga mkono jitohada za  Rais Samia Suluhu Hassan hususani katika kuwajali watoto nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Watoto hao wanaolelewa na Kituo cha Moyo wa Huruma kilichoazishwa na kufadhiliwa na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), walikuwa ni moja ya washiriki 61 waliopanda mlima Kilimanjaro tarehe 14 Julai 2023 na kushuka tarehe 20 Julai mwaka huu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama (katika) akiwa Abeli Mussa (kushoto) na Rebecca Damian (kulia) baada ya kuwapokea wanafunzi hao walioshiriki kupanda Mlima Kilimanjaro kupiti kampeni ya GGML KiliChallenge -2023 inayolenga kuhamasisha uchangishaji wa fedha za mapambano dhidi ya VVU/Ukimwi.

Washiriki hao walipanda mlima huo kupitia kampeni ya GGML KiliChallenge anayolenga kukusanya fedha za kuendeleza mapambano dhidi ya VVU/ Ukimwi.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya mashujaa juzi tarehe 25 Julai 2023 jijini Dodoma, Mhagama  alisema watoto hao walimuambia wamepanda mlima huo kwa kuzingatia kazi kubwa anayofanya Rais Samia Suluhu Hassan ya ulinzi wa watoto wa kitanzani, haki zao na ustawi wao.

“Vilevile kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya elimu ya msingi na sekondari na vyuo vikuu. Lakini pia wamesema walipanda kwa kuzingatia kazi kubwa unayofanya kwenye miundombinu ya afya haya yote yakiwa na ustawi mkubwa wa watoto wote wa Tanzania,” alisema.

Amesema mbali na kushirikiana na serikali kusaidia mapambano dhidi ya tatizo la Ukimwi, pia watoto hao ambao ni wanafunzi wa darasa la saba, walipanda mlima huo kwa lengo la kuanzisha moyo wa uzalendo kwa watoto wengine ili watambue kuwa nchi sasa inaoongozwa na rais ambaye anajali ustawi wa watoto.

Kati ya watoto hao, Rebecca Damiani ambaye ni mwanafunzi katika Shule ya Msingi Kivukoni- Geita, alifika katika kilele cha Uhuru cha mlima huo, huku Abel Mussa ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi Mbugani pia kutoka mkoani Geita, alirudia njiani baada ya kuugua malaria.

Kampeni hiyo iliyoasisiwa na GGML mwaka 2002 kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), mwaka huu ilishirikisha wapanda mlima 35 na waendesha baiskeli 26 waliouzunguka mlima Kilimanjaro kwa siku saba.

Akiwapokea washiriki hao, tarehe 20 Julai mwaka huu, Mhagama alimwagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhakikisha wanafunzi hao wanaingizwa kwenye orodha ya miongoni mwa watu watakaohudhuria sikukuu ya mashujaa ambayo imefanyika juzi tarehe 25 Julai 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!