Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watendaji kata, vijiji wanolewa matumizi mfumo wa kihasibu
Habari Mchanganyiko

Watendaji kata, vijiji wanolewa matumizi mfumo wa kihasibu

Spread the love

JUMLA ya watendaji 18 wa kata,  92 wa vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga wanatarajiwa kupatiwa mafunzo maalumu kuhusu matumizi ya Mfumo wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha (FFARS) kwa lengo la kuongesa kasi ya ukusanyaji mapato.

Mafunzo hayo ya siku mbili, yamefunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Khamis Katimba. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Khamis Katimba


Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo Katimba amewataka watendaji hao kusimamia vyema suala la ukusanyaji wa mapato katika maeneo yao.

“Watendaji wenzangu mpo hapa kupata mafunzo ya mfumo wa FFARS lakini niwaombe nendeni mkakusanye mapato, simamieni vyema hilo suala kwani ndiyo uti wa mgongo wa shughuli zote za serikali katika maeneo yenu,  hatuwezi kutekeleza shughuli yeyote kama hatuwezi kukusanya mapato. Simamieni kila kinachotakiwa kulipwa kiliipwe na  msioneee watu tendeni haki” amesema Ndugu Katimba.

Aidha, katika hatua nyingine Katimba amewataka watendaji hao kudumisha upendo miongoni mwa watumishi kwani wao ndio wasimamizi wakuu wa  watumishi katika maeneo yao na hivyo wanapaswa kuonesha dira nzuri  kwa watumishi wengine wanaowaongoza.

Nao baadhi ya watendaji wa kata na vijiji waliohudhuria mafunzo hayo wamempongeza Mkurugenzi huyo kwa kuendelea kufanya jitihada kubwa katika  kuimarisha ukusanyaji wa mapato ndani ya Halmashauri  huku pia wakimshukuru kwa kuendelea kuwa nao karibu na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!