Saturday , 30 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa 41 wafariki katika ajali ya Meli
Kimataifa

41 wafariki katika ajali ya Meli

Meli ya MV Liemba
Spread the love

AJALI ya meli iliyotokea karibu na nchi ya Italia kwenye kisiwa cha Lampedusa imesababisha vifo vya wahamiaji 41 huku wachache wakinusurika katika ajali hiyo. Anaripoti Mlelwa Kiwale, TUDARCo kwa msaada wa Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Manusura hao waliotoa ushuhuda wao kwenye ajali hiyo katika vyombo vya habari nchini humo, walikuwa kwenye boti iliyokuwa ikitokea nchini Tunisia jijini Sfax na kuelekea Italia ndipo boti hiyo ikazama.

Wahamiaji hao wanne walionusurika, walikuwa siyo wakazi wa Lampedusa bali ni watu wenye asili ya kutoka Guinea na Ivory Coast.

Aidha, taarifa zinaeleza kuwa wahamiaji haramu huwa wanapitia katika lango maarufu la bandari lililo karibu na Lampedusa kwa lengo la kutafuta maisha yaliyo mazuri nchini humo.

Pia vikundi vya uokoaji na boti za doria za Italia zimekuwa zikitoa msaada na kuokoa watu takribani 2,000 ambao walifikia nchini humo.

Hata hivyo, unaelezwa watu 1,800 waliovuka kutoka Afrika Kaskazini na kuelekea Ulaya wamepoteza maisha ndani ya mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!