Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watatu wachukua fomu za urais Tanzani
Habari za Siasa

Watatu wachukua fomu za urais Tanzani

Mutamwega Bati Mgaiwa wa SAU
Spread the love

WAGOMBEA watatu wamechukua fomu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kugombea Urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Wagombea hao wamekabidhiwa fomu hizo leo Jumatano tarehe 5 Agosti 2020 na Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC katika ofisi za tume hiyo zilizoko Ndejengwa jijini Dodoma.

Waliochukua fomu ni, Seif Maalim Seif wa Chama cha Alliance for African Farmers Party (AAFP), aliyeambatana na mgombea Mwenza, Rashid Ligania Rai.

Philipo John Fumbo wa Chama cha Democratic Party (DP) na Leopold Mahona wa Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA), aliyeambatana na Mgombea Mwenza Hamis Alli Hassan.

         Soma zaidi:-

Wagombea hao wamechukua fomu hiyo siku ya kwanza baada ya zoezi hilo kufunguliwa leo. Zoezi hilo litafungwa tarehe 25 Agosti 2020.

Akizungumza baada ya kuwakabidhi fomu hiyo, Jaji Kaijage amewataka wagombea hao kurejesha fomu kwa wakati husika kwa ajili ya kupisha zoezi la uteuzi wa wagombea Urais wa Tanzania katika uchaguzi huo.

“Itakapofika siku ya uteuzi tarehe 25 Agosti, 2020 mtarejesha fomu zenu hapa Tume na Tume baada ya kujiridhisha kuwa mnazo sifa itafanya uteuzi,” amesema

Jaji Kaijage amewapongeza wagombea hao kwa kuchukua fomu, akisema kwamba ushiriki wao utachangia kudumisha demokrasia nchini.

“Ninawapongeza kwa kutumia haki yenu ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa. Ushiriki wenu utachangia kudumisha demokrasia nchini mwetu na ninawatakia kila la heri,” amesema Jaji Kaijage.

Kesho Alhamisi, Rais John Magufuli, Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) atakwenda kuchukua fomu hizo huku Jumamosi tarehe 8 Agosti, 2020, mgombea wa Chadema, Tundu Lissu atakwenda kuchukua fomu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!