Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanafunzi wa TUDARCo wamuunga mkono Rais Samia
Habari Mchanganyiko

Wanafunzi wa TUDARCo wamuunga mkono Rais Samia

Spread the love

 

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini mkoani Dar es Salaam (TUDARCo) wameunga mkono juhudi za Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hasssan kwa kutembelea mapango ya Amboni yaliyopo mkoani Tanga kwa lengo la kujionea mambo mbalimbali na mengine yakiwa ya ajabu. Anaripoti Victoria Mwakisimba, TUDARCo … (endelea).

Rais Samia ambaye aliamua kutengenezwa na filamu ya utalii ya “The Tanzania Royal Tour” ikiwa na lengo la kuhamasika na utalii wa nje na ndani ya nchi ikiwemo kuzuru maeneo mbalimbali ya utalii na hata ya makumbusho ya kihistoria.

Wanafunzi hao wanaosomea shahada ya mawasiliano ya Umma katika chuo hicho wamechukua maamuzi hayo ya kutembelea mapango hayo ili kumuunga mkono Rais Samia na kuwa kama mfano kwa wanafunzi wengine kutembelea katika vivutio mbalimbali vya utalii nchini .

Mmoja kati ya waandishi waliotembelea mapango hayo, Isack Yohana alisema; “Wengi wetu ikiwa ni mara ya kwanza kutembelea mapango ya Amboni tumejionea mambo ya ajabu ambayo tungesimuliwa tungedhani hayana  ukweli wowote.

“Tumeonyeshwa njia mbili moja ikiwa ni ya mizimu na nyingine ikiitwa njia ya uzima, lakini pia tumeona mapango yenye picha ya bikira Maria. Kwetu hiki ni kitu kikubwa sana kwani tumepata ushuhuda ambao umeongeza kitu katika elimu yetu.”

Alisema ndani ya mapango ya Amboni kuna vitu vingi vinavyoibua udadisi na vinavutia, ikiwemo njia ya uzima ambayo ni nyembamba lakini mtu hata akiwa mnene sana anapita bila shida.

Kwa upande wake, Abraham Manfred alisema kutokana na umbo lake la unene aliamini hawezi kupita katika njia ya uzima lakini alistahajabu alivyoweza kupita katika njia hiyo.

“Mwongozaji alipotoa maelekezo nilihisi haikuwa kweli lakini niliweza kupita kwenye njia hiyo nyembamba bila shida yoyote wala kukwama mpaka mwisho,” alisema Abraham.

Maajabu mengine ambayo yapo katika mapango ya Amboni ni uwepo wa giza nene kiasi hata watu wakiwa wawili wameshikana mikono bila taa hawawezi kuonana na hata wakivaa nguo nyeupe bado hawawezi kuonekana bila mwanga wa taa.

Aidha kuna jumla ya mapango saba lakini waongozaji wamepewa ruhusa ya kuwaonyesha watalii mapango manne tu.

Ni wakati wa watanzania kuamka sasa na kulitangaza taifa kimataifa na kuunga mkono juhudi za Rais Samia katika kukuza sekta ya utalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!