KATIKA kuunga mkono agenda ya kusaidia matibabu ya Fistula kwa kina mama wasio na uwezo, wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania hii leo tarehe 25 Septemba 2021, wameungana na maelfu ya watanzania wengine akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kushiriki mbio za Hisani za NMB Marathon. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mbio hizo zilikuwa na kauli mbiu ‘Mwendo wa Upendo,’ zikilenga kukusanya kiasi cha Sh . 1 bilioni ili kufanikisha mpango huo.
Mbali na kushiriki mbio hizo Benki hiyo pia ilitoa mchango wa fedha kiasi cha Sh Mil 10 kwa waandaaji wa mbio hizo ili kuunga mkono jitihada hizo.
Leave a comment