Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge, Spika watoa Sh. 100 milioni kwa wafiwa
Habari za Siasa

Wabunge, Spika watoa Sh. 100 milioni kwa wafiwa

Job Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Kongwa
Spread the love

WABUNGE wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameadhimia kutoa milioni 86 pesa za posho ya kikao cha siku kwa ajili ya rambirambi kwa familia za wafiwa, wanafunzi na wafanyakazi wa shule ya msingi Lucky Vincent Academy mkoani Arusha, anaandika Hamisi Mguta.

Job Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania, amesema wabunge wamekubaliana kutoa posho zao za siku ya leo kupeleka kwa familia za wafiwa kama rambirambi zao, marehemu waliopoteza maisha katika ajali mkoani humo.

“Tumekubaliana kwa kauli moja humu bungeni tutoe posho ya siku moja kama rambirambi yetu, posho hiyo tutaipeleka mara moja kwa Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo na itagawiwa sawa sawa kwa wafiwa wote,”amesema Ndugai.

Kiasi cha rambirambi kinachotolewa na Bunge ni Sh. 100 milioni ambapo amefafanua kuwa Sh, 86 milioni zinatokana na posho hizo za kikao cha siku moja na Sh. 14 milioni zimetoka katika Ofisi ya Spika.

Tazama video chini, Job Ndugai akifafanua juu ya rambirambi hizo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!