Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge, Spika watoa Sh. 100 milioni kwa wafiwa
Habari za Siasa

Wabunge, Spika watoa Sh. 100 milioni kwa wafiwa

Job Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Kongwa
Spread the love

WABUNGE wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameadhimia kutoa milioni 86 pesa za posho ya kikao cha siku kwa ajili ya rambirambi kwa familia za wafiwa, wanafunzi na wafanyakazi wa shule ya msingi Lucky Vincent Academy mkoani Arusha, anaandika Hamisi Mguta.

Job Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania, amesema wabunge wamekubaliana kutoa posho zao za siku ya leo kupeleka kwa familia za wafiwa kama rambirambi zao, marehemu waliopoteza maisha katika ajali mkoani humo.

“Tumekubaliana kwa kauli moja humu bungeni tutoe posho ya siku moja kama rambirambi yetu, posho hiyo tutaipeleka mara moja kwa Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo na itagawiwa sawa sawa kwa wafiwa wote,”amesema Ndugai.

Kiasi cha rambirambi kinachotolewa na Bunge ni Sh. 100 milioni ambapo amefafanua kuwa Sh, 86 milioni zinatokana na posho hizo za kikao cha siku moja na Sh. 14 milioni zimetoka katika Ofisi ya Spika.

Tazama video chini, Job Ndugai akifafanua juu ya rambirambi hizo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!