Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Wabunge kuminyana uchaguzi Simba
Michezo

Wabunge kuminyana uchaguzi Simba

Juma Nkamia
Spread the love

KAMATI ya uchaguzi ya klabu ya Simba imewapitisha Juma Nkamia na Murtaza Mangungu kuwania nafasi ya Mwenyekiti katika uchaguzi mdogo wa klabu hiyo mara baada ya kupita katika michakato yote. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Uchaguzi huo ambao utafanyika tarehe 7 Februari, 2021 ambao utakuwa wa kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Swedi Nkwabi ambaye alijiuzuru katika nafasi hiyo 14 septemba 2019.

Wagombea hao ambao walikuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania katika muhura uliopita ambao Juma Nkamia akiwakilisha jimbo la Chemba (CCM) lililopo Dodoma, huku Murtaza Mangungu akiwakilisha jimbo la Kilwa Kaskazini.

Akitangaza majina hayo mbele ya waandishi wa habari leo tarehe 16 Januari, 2021 kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Boniface Lihamwike alisema kuwa wawili hao wamepitishwa kutokana na wagombea wawili kujitoa kwenye kinyang’anyiro hicho kutokana na sababu zao binafsi mara baada ya kupitia kwenye hatua ya pingamizi.

“Wakati tukiwa na wagombea hawa wanne kamati yangu ilipokea barua kutoka kwa wagombea wawili ambao ni Rashidi Shangazi pamoja na Hamisi Omari wakiomba kujiengua kwenye mchakato huu kwa kuwa sehemu ya wagombea,” alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha Lihamwike aliendelea kwa kusema kuwa mara baada ya kuleta maombi hayo ya kutaka kujiengua kwenye uchaguzi huo kamati ilikaa na kuwapa majibu ya kukubali maombi yao kwa kuwa ni jambo lililopo kwenye kanuni.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo aliwataka wanachama wa klabu ya Simba kuwapa ushirikiano wagombea hao na kuwataka kufanya kampeni za kistaarabu huku wakizingatia kanuni za uchaguzi na sheria za nchi na kama kuna mgombea akikiuka kanuni hizo atachukuliwa hatua stahiki.

Murtaza Mangungu

“Nawahasa wagombea hawa ambao wamepita, kufanya kampeni kistaarabu kwa kuzingatia sheria za nchi na kanuni za uchaguzi na kamati yangu haitasita kumchukulia mgombea hatua kama atakwenda tofauti na taratibu,”  aliongezea Mwenyekiti huyo.

Toka kuanza kwa mchakato huo wa uchaguzi ndani ya Simba toka tarehe 13 Desemba, 2020 wanachama waliojitokeza kuchukua fomu walikuwa 11 na fomu zilizorejeshwa zilikuwa saba, na mara baada ya kamati hiyo kufanya upembuzi walifanikiwa kupitisha majina matono.

Kampeni za uchaguzi huo zitadumu kwa siku 21, ambazo zinaanza kuanzia siku ya kesho tarehe 17 Januari, 2021 mpaka tarehe 6 Februari, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!