Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Vyeti bandia vyazidi kutikisa
Habari MchanganyikoTangulizi

Vyeti bandia vyazidi kutikisa

Spread the love

WANANCHI wamewataka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita), pamoja na Wizara ya Elimu Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, wabuni njia mbadala ya kudhibiti matumizi ya vyeti bandia katika mfumo wa utoaji elimu, anaandika Faki Sosi.

Hayo yamesemwa ikiwa ni siku chache baada ya serikali chini ya Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) kuanzisha utaratibu mpya wa kuzuia wanafunzi wasio na vyeti vya kuzaliwa kutofanya mitihani ya darasa la nne na saba kwa lengo la kukomesha watumiaji wa majina na vyeti feki vya watu wengine.

Wananchi hao wametoa kauli hiyo leo walipokuwa wakizungumza na MwanaHALISI Online ambapo kwa wakati tofauti wamesema kuwa vyeti vya kuzaliwa ni muhimu na serikali na mawakala wake walitakiwa kujua umuhimu wa jambo hili mapema.

Saidi Lubago mkazi Kinondoni, Dar es Salaam amesema kuwa Rita wangeweza kurekebisha mfumo wao wa utoaji vyeti.

“Itakuwa wamechelewa kwa sababu tayari wapo wangine watu wazima hawana vyeti vya kuzaliwa hivyo mfumo huo ungeanza mapema,” amesema Lubago.

Mariamu Hussein mkazi wa Kinondoni, Dar es Salaam, amesema kuwa yupo yeye amepata usumbufu katika kutafuta cheti cha mtoto wake kutokana na watendaji wa Rita kutokamilisha zoezi hilo mapema ambapo yeye alishindwa kwenda kila siku kuhangaikia vyeti na kuacha kutafuta riziki.

Juzi, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Rita, Emmy Hudson alisema kuwa utaratibu huo mpya ni agizo la serikali lenye lengo la kuweka kumbukumbu sahihi za wanafunzi kuanzia ngazi ya chini na kukwepa udanganyifu wa majina na vyeti.

“Tayari juhudi mbalimbali zimechukuliwa ili kupunguza msongamano katika ofisi zao za kupata vyeti hivyo na tumeanza kuvitolea shuleni”.

Hivi karibuni kabla ya mfumo huo kutangazwa rasmi, kumekuwepo na taarifa za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutumia jina na cheti cha mtu mingine kujiendeleza kielimu huku jina lake halisi likielezwa kuwa ‘Daud Albert Bashite’.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!