Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Viongozi wa dini wavutana mbele ya Rais Magufuli
Habari za Siasa

Viongozi wa dini wavutana mbele ya Rais Magufuli

Askofu Josephat Gwajima
Spread the love

ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mchungaji Amani Lyimo amevutana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima kuhusu usajili wa makanisa hapa nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza katika Mkutano wa Viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali na Rais John Magufuli, Mchungaji Lyimo amedai kuwa, sasa hivi injili imekuwa biashara na kuitaka serikali kudhibiti usajili wa makanisa kwa kuanzisha kamati maalumu itakayosimamia usajili na maadili ya makanisa hayo.

Mchungaji Lyimo amesema kuwa “Kama mtakumbuka viongozi wa dini kipindi cha uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere ilikuwa dini au dhehebu jipya linaanza, kabla ya kusajiliwa, viongozi wa dini wanajadili hilo dhehebu , wanapeleka maoni yao wizara ya mambo ya ndani kisha linasajiliwa, sasa hivi kuna makanisa mengi, injili imekuwa biashara.

Kuwe na kamati maalum ambayo itashughulikia usajili wa viongozi wa dini, hekima za wazee zinaweza kutumika katika kusuajili wakishirikiana na watendaji wao.”

Akijibu kuhusu pendekezo hilo, Askofu Gwajima amesema si sahihi kwa serikali kubana makanisa kwa kuwa uwepo wa madhehebu mengi yanayohubiri injili inavyotakiwa inakuwa Baraka kwa nchi.

“Pastor Lyimo amemaliza kuzungumza nikaona akasema ni muhimu serikali ifanye utaratibu kuwa mgumu, nina fikiri jambo hilo si sahihi, sababu ziko nyingi sana, ukienda kila mahali hatua moja utakuta baa hatua moja grosari, sehemu nyingine haina baa watu wanakunywa pombe.

Madhehbu yanayohubiri sawa sawa injili yanapokuwa mengi inakuwa Baraka kwa nchi, nimshauri kwamba madhehebu yasipunguwe isipokuwa yaongezeke na kuhubiri yanayotakiwa kuhubiriwa,” amesema Askofu Gwajima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!