Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Viongozi 140 waiandikia barua WHO kutaka dawa ya corona iwe bure 
Habari Mchanganyiko

Viongozi 140 waiandikia barua WHO kutaka dawa ya corona iwe bure 

Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini
Spread the love

RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa na Imran Khan, Waziri Mkuu ni miongoni mwa viongozi 140 waliosaini barua kwenda Shirika la Afya Duniani (WHO), wakishauri dawa ya corona itakapopatikana, igawiwe bure kwa watu wote. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Wamesema, dawa pamoja na chanjo yake inapaswa kugawiwa bure, na iwe haki ya kila mwanadamu kupata dawa hiyo ili aishi.

“Dawa ya corona haipaswi kuwa biashara duniani, wanasayansi watakaovumbua wawaeleze wanasayansi wenzao namna ya utengeneza.”

“Serikali za mataifa lazima ziungane duniani kote ili kuhakikisha kwamba, pale dawa itapopatikana, inazalishwa kwa wingi na haraka na zinasambazwa kwa watu wote, katika mataifa yote bila malipo,” barua hiyo imeeleza, na kuongeza:

“Tiba, utambuzi na uvumbuzi wowote ulio na uhusiano na CIVID-19, unapaswa kuelezwa kwa mataifa yote bila ubaguzi.”

Pia, Rais Ramaphosa jana jioni Jumatano tarehe 13 Mei 2020, alipohutubia taifa hilo alisema, nchi yake licha ya maambukizi kufika 12,000, bado mpango wa kuondoa vikwazo vya kukaa ndani unaendelea na anatarajia mwishoni mwa mwezi huu, watu wataendelea na shughuli zao kama kawaida.

Ramaphosa alisema, “baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa zaidi na COVID-19 nchini humo yataendelea na utaratibu wa kujifungia mpaka maambukizi yatakapopungua.”

Mpaka tarehe ya leo, Afrika Kusini imeshuhudia vifo 219 vilivyotokana na ugonjwa wa corona.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!