MKAGUZI Mkuu wa Ndani wa Benki ya NMB, Benedicto Baragomwa alikuwa miongoni mwa viongozi walioshiriki kilele cha mbio za mwenge kitaifa 2022, katika uwanja wa Kaitaba Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Mbio hizo zilihitimishwa Oktoba 14, 2022 na mgeni rasmi alikuwa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Katika uwanja huo, Baragomwa akiwa na Meneja wa NMB kanda ya Ziwa Baraka Ladislaus kwa pamoja walipata fursa ya kuteta na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022, Sahili Nyanzabara Geraruma kwenye maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge huo katika uwanja wa Kaitaba Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.
Leave a comment