Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tunduma watenga milioni 377 kununua gari la zimamoto
Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga milioni 377 kununua gari la zimamoto

Spread the love

KATIKA kukabiliana na majanga ya moto, Halmashauri ya mji Tunduma mkoani Songwe umetenga Sh 377 milioni za mapato ya ndani kununua gari la zima moto. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Akizungumza leo tarehe 10 Julai 2023 ofisini kwake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Phillimon Magesa amesema kutokana na mji wa Tunduma kukua kwa kasi huku ujenzi wa masoko  ukiongezeka, wameamua kununua gari la zima moto kujikinga na majanga ya moto pindi yatakapotokea.

Amesema gari hilo lenye thamani ya Sh 377 milioni, wamepanga kulipa kwa awamu tatu kupitia fedha za mapato ya ndani.

Amesema kwa kuanzia wamelipa  Sh 130 milioni lengo ikiwa ni kuhakikisha wafanyabiashara wanaokolewa bidhaa zao pindi zitokeapo ajili za majanga ya moto.

Amesema mbali na gari hilo la zima moto pia wametenga Sh. 6 milioni kununua gari litakalokuwa likifanya kazi ya kutembelea miradi ya halmashauri hiyo.

Pia amesema wanaendelea na mipango ya kufungua kampuni itakayofanya kazi hiyo ya usimamizi wa vitega uchumi vya halmashauri.

Amesema kutokana na uwepo wa mipango hiyo, wanataka kuunda kampuni au chombo (Special purpose vehicle (SPV) kitakachosimamia shughuli mbalimbali zikiwemo za kibiashara na uzalishaji.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Ayoub Mlimba amesema nia ya baraza la madiwani kupitisha manunuzi hayo ni kutaka mali za wafanyabiashara na wawekezaji wa miradi mbalimbali kuwa salama na kuwavuta wawekezaji wengi kuja kuwekeza Tunduma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!