Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TMA yatoa ufafanuzi ya Kimbunga Freddy
Habari Mchanganyiko

TMA yatoa ufafanuzi ya Kimbunga Freddy

Spread the love

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa ufafanuzi juu ya taarifa za uwepo wa kimbunga “Freddy” zinazosambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kuzua taharuki kwa jamii. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na TMA, imesema kuwa kupitia sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Na. 2 ya mwaka 2019, Mamlaka imepewa jukumu kisheria kufuatilia na kutoa tahadhali za hali mbaya ya hewa kwa jamii. Taarifa hizi za hali mbaya ya hewa hutolewa kwa jamii pale tu zinapokuwa zimekidhi viwango na miongozo ya utendaji kazi.

Kwa takribani wiki sasa Mamlaka imekuwa ikifuatilia mwenendo wa kimbunga “Freddy” kilichopo kusini magharibi mwa bahari ya Hindi karibu na pwani ya Madagascar na kujiridhisha kutokuwa na madhara ya moja kwa moja kwa sasa kwa maeneo yaliyoko nchini kwetu.

Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania, inaendelea kufuatilia kwa kina mwenendo wa kimbunga hiki na itatoa taarifa punde tu kutakapokuwa na haja ya kufanya hivyo.

Aidha, Mamlaka inapenda kuikumbusha jamii na umma kwa ujumla kuwa kwa mujibu wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Na. 2 ya 2019, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ndiyo pekee yenye mamlaka ya kutoa taarifa za tahadhari za matukio ya hali mbaya ya hewa na ni kosa kisheria mtu mwingine kufanya hivyo.

Kwa taarifa hii wananchi wanashauriwa kuendelea kuzingatia taarifa na tahadhari za hali mbaya ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania sambamba na kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazotokana na hali mbaya ya hewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!