Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko TEF yawatuliza wadau wa habari marekebisho vifungu kandamizi
Habari Mchanganyiko

TEF yawatuliza wadau wa habari marekebisho vifungu kandamizi

Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile
Spread the love

 

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF), limewataka wadau wa habari nchini kuwa na subira kwa kuwa muswada wa mabadiliko ya Sheria ya Huduma za Habari ya 2016, utawasilishwa bungeni kwa ajili ya kufanyiwa kazi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 3 Februari 2023 na Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, baada ya baadhi ya wadau kuhoji kwa nini ratiba ya vikao vya mhimili huo haijaweka wazi lini muswada huo utawasilishwa bungeni.

Balile amesema muswada huo haujawekwa kwenye ratiba moja kwa moja kwa kuwa, utawasilishwa bungeni kupitia marekebisho madogo ya sheria mbalimbali.

“Muswada utaingia bungeni katika kikao cha Bunge kinachoendelea sasa , nimetoa taarifa hii sababu nimeona watu wengi wanaangalia ratiba ya bungeni wananipigia simu vipi mbona haumo kwenye sheria zitakazojadiliwa. Lakini mimi nina taarifa za uhakika kwamba mpaka jana jioni kulikuwa na kila dalili kwamba utaingizwa bungeni,” amesema Balile na kuongeza:

“Isipokuwa kitakachobadilika nadhani hatutaona ule muswada kwa njia ya kawaida ambapo unapelekwa muswada unaojitegemea kama ilivyo kwa bima ya afya, kitakachotokea muswada utaingia katika utaratibu wa marekebisho madogo madogo ya sheria mbalimbali. Tuendelea kusubiria maana tunaendelea kuwasiliana na Serikali na watunga sera kuona jinsi gani itakavyokwenda.”

Hivi karibuni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, alisema muswada huo uliolenga kufanya marekebisho dhidi ya vifungu vinavyolalamikiwa na wadau kuwa vinakandamiza uhuru wa tasnia hiyo, ulishindwa kuwasilishwa bungeni Novemba mwaka jana ili kutoa nafasi ya kutosha kupokea maoni ili ipatikane sheria bora zaidi.

Nape alisema kwamba mapendekezo ya wadau kuhusu marekebisho hayo yalifikishwa katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kwa ajili ya kupitiwa ili muswada wake uwasilishwe bungeni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!