Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yayumba vivutio vya asili
Habari Mchanganyiko

Tanzania yayumba vivutio vya asili

Spread the love

SERIKALI imetaja sababu za Tanzania kushuka kwa nafasi tano, kutoka nafasi ya pili hadi ya nane katika orodha ya nchi zenye vivutio vya asili duniani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akijibu swali la Mbunge wa Vunjo, James Mbatia leo tarehe 21 Mei 2019 bungeni jijini Dar es Salaam, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamiss Kigwangalla amesema Tanzania imeshuka kutokana na uharibifu wa mazingira katika maeneo ya vivutio vya utalii.

Katika swali lake, Mbatia ameuliza Tanzania inashika nafasi ya ngapi kwenye orodha ya nchi yenye vivutio vya asili na miundombinu mizuri ya kuvutia watalii duniani?

Dk. Kigwangalla amesema, uharibifu wa mazingira na uvamizi wa mifugo pamoja na shughuli za kibinadamu katika maeneo ya vivutio ndiyo chanzo cha Tanzania kushuka, na kwamba kwa sasa serikali inakabiliana na changamoto hiyo.

“Utafiti uliofanyika mwaka 2012 hadi 2014 ulitoa taarifa kuwa, Tanzania inashika nafasi ya pili kwa vivutio vya asili duniani. Kutokea kipindi hicho hadi sasa haujafanyika utafiti mwingine, lakini matokeo ya katikati yalitoka ilionekana imeshuka kutoka nafasi ya 2 hadi 8,” amesema Dk. Kigwangalla na kuongeza;

 “Sababu uharibifu wa mazingira, uvamizi wa mifugo na makazi katika maeneo ya vivutio vya utalii vya asili. Kazi kubwa kuondoa wavamizi na kupandisha hadhi maeneo, inaweza ikapandisha zaidi kwenye ubora wa vivutio vya utalii duniani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!