Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania, DRC zakubaliana kuboresha miundombinu
Habari Mchanganyiko

Tanzania, DRC zakubaliana kuboresha miundombinu

Spread the love

SERIKALI za Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwa pamoja zimeingia makubaliano ya  kuboresha miundombinu ya barabara, reli na bandari ili kuongeza ufanisi katika biashara na hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hafla ya makubaliano hayo imefanyika jijini Dar es Salaam jana tarehe 9 Novemba, 2022 ambapo Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Tanzania, Prof. Makame Mbarawa amesema makubaliano yataimarisha miundombinu ya reli, barabara, bandari na ujenzi wa meli za mizigo na abiria.

“Tunakusudia kuongeza ufanisi wa kibiashara katika nchi zetu na hivyo kuimarisha uhusiano wa kindugu na kukuza uchumi wa nchi zetu”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Prof. Mbarawa amesema miradi hiyo ambayo ujenzi wake utatekelezwa kwa awamu utapunguza muda wa safari kutoka DSM kwenda Lubumbashi nchini DRC na hivyo kupunguza gharama za biashara na muda wa kusafirisha mizigo toka siku 30 hadi wiki moja.

Waziri wa Miundombinu wa DRC, Alexis Mavunyi amesema namna mataifa hayo mawili yatakavyo nufaika kutachochea uzalishaji wa bidhaa, mazao na biashara zingine hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo na raia wao.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ushoroba wa Kati, Wakili Froly Okanju amesema  makubaliano hayo yatafungua fursa kubwa ya usafirishaji kwa nchi za ushoroba wa kati ambazo zinakwenda kupata maendeleo kwa kuwa zinaitegemea Tanzania katika uingizaji wa mizigo na hivyo kuitaka Tanzania kujipanga kuhudumia nchi za ushoroba huo kikamilifu.

Pamoja na mambo mengine ujenzi wa Miradi hiyo inayotarajiwa kuanza utekelezaji wake baadae mwakani itatoa fursa kwa Serikali za Tanzania, DRC, Wadau wa Maendeleo ya kuzalisha nafasi za ajira.

Viongozi hao pamoja na ujumbe wao wametembelea Shirika la Reli TRC na Mamlaka ya Bandari nchini TPA na kufurahishwa na namna taasisi hizo zinavyofanya kazi kwa weledi na ubunifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!