SPIKA wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson, ameutaka Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), usikae kimya katika kuwaeleza wananchi maendeleo yanayofanywa na Serikali, kwani kitendo hicho kitawalinda viongozi walioko madarakani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Spika Tulia ametoa wito huo leo tarehe 26 Novemba 2022, akizungumza katika matembezi ya UVCCM yaliyofanyika jijini Dodoma.
“Niwaombe sana kuja kwetu hapa kuwe ni chachu ya hamasa, mrejeapo kwenye mikoa yenu mkaendeleze mazoezi kusema kazi nzuri zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, mkaendelee kueleza kazi nzuri zinazofanywa na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi. Msikae kimya waelezeni wananchi,” amesema Spika Tulia.
Aidha, Spika Tulia amewataka vijana wa UVCCM kuwa wa kwanza kuanzisha hoja, badala ya kusubiri wengine kutoka vyama vya upinzani kuanzisha masuala aliyoyaita kuwa ni vioja.
“Tusisubiri wenzetu waanzishe vioja halafu ndiyo tufanye kazi ya kuwajibu, anzisha wewe hoja wakibisha wape data. Sisi sio watu wa kuanzishiwa vioja halafu tuanze kubisha, sisi kazi yetu kuanzisha hoja, walete vioja tuwape hoja,” amesema Spika Tulia.
Spika Tulia amewataka vijana wa CCM kueleza miradi ya maendeleo inayotoekelezwa na Serikali katika maeneo yao ili wananchi wapate kuelewa kazi inayofanywa na viongozi.
Asante ndugu tullia kwa habari njema