Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa BAVICHA kuongoza vijana wa vyama vya demokrasia Afrika
Habari za Siasa

BAVICHA kuongoza vijana wa vyama vya demokrasia Afrika

Spread the love

BARAZA la Vijana la Chama cha Chadema (BAVICHA), litaongoza Umoja wa Vijana wa Afrika kutoka vyama vya kidemokrasia (YDUA), katika kipindi cha mwaka mmoja (2022-2023), kupitia mjumbe wake Gwamaka Mbugi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ni baada ya Mbugi aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa YDUA, kuteuliwa kuwa Mwenyekiti akishika nafasi ya Louisa Atta-Agyewang, aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia Afrika (DUA).

Akizungumza na wanahabari jana tarehe 26 Novemba 2022, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano BAVICHA, Apolinary Boniface, amesema hatua hiyo ni fursa kwa vijana wa Chadema na taifa kwa ujumla.

“Bavicha tunajivunia kuongoza taasisi kubwa hii vijana Afrika, ambayo itakuwa fursa kubwa chama, vijana na taifa kwa ujumla.Tunampongeza na kumtakia heri Gwamaka Mbugi katika kuongoza taasisi hiyo muhimu kwa vijana. Bavicha tutaitumia fursa hiyo kusukuma agenda za vijana,” amesema Boniface.

Boniface amesema kuwa siyo mara ya kwanza kwa Bavicha kuongoza nafasi za kimataifa.

“Bavicha tunaongoza nafasi zingine kimataifa, Dorcas Francis kutoka Bavicha ni Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Vyama vya kidemokrasia Duniani (IYDU). Pia Hellen Sisya ni Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Umoja wa Vijana wa Vyama vya Kidemokrasia Afrika (YDUA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!