Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yatumia dakika 3 kuwaua Wabotswana
Michezo

Simba yatumia dakika 3 kuwaua Wabotswana

Spread the love

 

DAKIKA tatu zimetosha kwa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2020/21, Simba kuanza safari vyema ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika kwa kuibuika na ushindi wa 2-0 dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Mchezo huo wa awali, umechezwa leo Jumapili katika Uwanja wa Taifa wa Botswana ukishuhudia vijana hao wa Msimbazi jijini Dar es Salaam, wakitumia dakika tatu za kipindi cha kwanza kujinyakulia ushindi huo muhimu.

Alikuwa ni kiungo mkabaji raia wa Uganda, Thadeo Lwanga aliyeifungia Simba bao la kwanza dakika ya tatu kipindi cha kwanza, baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Galaxy na yeye kupiga shuti kali.

Dakika tatu baadaye yaani dakika ya sita, nahodha wa kikosi hicho, John Bocco aliindikia Simba bao la pili kwa shuti kali na hadi dakika 90 zinamalizika, Simba wametoka kifua mbele.

Mchezo wa pili wa marudiano, utapigwa wiki moja baadaye katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam. Ikiwa Simba itashida au kutoka sare mchezo huo, utawapeleka hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Ili Galaxy iitoe Simba, itahitaji kushinda magoli 3-0 katika Uwanja wa Mkapa au 4-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!