Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto
Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the love

SUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu, ikiwa ni hatua ya tahadhari kutokana na joto kali linalotarajiwa kudumu kwa wiki mbili. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Wizara za afya na elimu zimetoa ushauri kwa wazazi kuwabakisha watoto wao nyumbani, kwa sababu viwango vya joto vinatarajiwa kufikia nyuzi 45.

Serikali imesema shule yoyote itakayokiuka agizo hilo na kuendelea kufungua wakati wa kipindi cha tahadhari itafutiwa usajili wake.

Hata hivyo, tahadhari hiyo iliyotolewa usiku wa kuamkia Jumapili haikufafanua ni kwa muda gani shule zitafungwa.

Sudan Kusini, taifa changa zaidi barani Afrika linakabiliwa na hatari ya athari ya mabadiliko ya tabia nchi na joto kali. Lakini ni nadra sana kwa viwango vya joto nchini humo kupita nyuzi 40 katika vipimo vya Celsius.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!