Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Serikali yakadiria bajeti ya Sh 44.3Tril. mwaka 2023/24
Habari Mchanganyiko

Serikali yakadiria bajeti ya Sh 44.3Tril. mwaka 2023/24

Spread the love

 

SERIKALI imewasilisha kwa Wabunge Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/24, ambapo imepanga kukusanya na kutumia jumla ya Sh. 44.3 trilioni. Anaripoti Mwandishi Wetu Dodoma … (endelea).

Bajeti hiyo inajumuisha Sh. 29.2 trilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh 15.1 trilioni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Akiwasilisha mapendekezo hayo leo Jumatatu tarehe 13 Machi, 2023 jijini Dodoma Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema kiasi hicho ni sawa na ongezeko la asilimia 7 ikilinganishwa na bajeti iliyoidhinishwa na Bunge ya mwaka wa Fedha 2022/23 ya Sh. 41.5 trilioni.

Amesema jumla ya mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa Sh. 31 trilioni , sawa na asilimia 70.7 ya bajeti yote ambapo kati ya mapato hayo, mapato yanayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yanakadiriwa kuongezeka kwa asilimia 13.0 hadi Sh. 26.7 trilioni kutoka makadirio ya Sh.23.7 trilioni mwaka 2022/23.

“Misaada na mikopo nafuu kutoka kwa Washirika wa Maendeleo inatarajiwa kufikia Sh. 5.4 trilioni, sawa na asilimia 12.3 ya bajeti yote,” amesema Dk. Nchemba.

Dk. Nchemba amesema Serikali inatarajia kukopa Sh. 5.4 trilioni kutoka soko la ndani ambapo Sh. 3.5 trilioni ni kwa ajili ya kulipia hatifungani na dhamana za Serikali zinazoiva na Sh. 1.9 trilioni kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Ameongeza kuwa Serikali inatarajia kukopa Sh. 2.1 trilioni kutoka soko la nje kwa masharti ya kibiashara ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu.

Kuhusu mgawanyo wa matumizi, Dk. Nchemba alisema kuwa kati ya fedha hizo, Sh. 29.2 trilioni zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikijumuisha Sh. 12.8 trilioni kwa ajili ya ulipaji wa deni la Serikali na gharama nyingine za Mfuko Mkuu na Sh. 10.9 trilioni kwa ajili ya mishahara ikiwemo upandishaji wa madaraja kwa watumishi na ajira mpya, na Sh. 6.4 trilioni kwa ajili ya matumizi mengineyo (OC).

“Matumizi ya maendeleo yanatarajiwa kuwa shilingi trilioni 15.1 ambapo kati ya kiasi hicho, shilingi trilioni 11.9 ni fedha za ndani, sawa na asilimia 78.3 ya bajeti ya maendeleo na shilingi trilioni 3.2 ni fedha za nje”, ameongeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!