Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ataka vifungu vinavyowabana vijana kugombea uongozi viondolewe
Habari za Siasa

Ataka vifungu vinavyowabana vijana kugombea uongozi viondolewe

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama cha ACT-Wazalendo, Mkoa wa Dar es Salaam, Felix Kamugisha, ameitaka Serikali kurekebisha vifungu vinavyozuia vijana wenye umri chini ya miaka 20 kugombea nafasi za uongozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kamugisha ametoa wito huo wakati akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), jana tarehe 12 Machi 2023.

Alisema kuwa, Sheria ya Uchaguzi imemnyima kijana mwenye umri kuanzia miaka 18 hadi 20 kupigiwa kura, wakati mwenye umri kuanzia miaka 18, anaruhusiwa kupiga kura.

“Sheria ya Uchaguzi inamtaka kijana mwenye umri wa miaka 18 kupiga kura lakini inamnyima haki ya kupigiwa kura kwa maana kugombea ubunge na udiwani hadi ufikie umri wa miaka 21. Vijana wengi wenye uwezo na sifa za kuwa kiongozi kuwa nyuma ya wagombea kuwachorea ramani na mikakati ya ushindi,” alisema Kamugisha.

Mwenyekiti huyo wa vijana ACT-Wazalendo Dar es Salaam, amewataka vijana kupaza sauti zao ili mfumo unaotenga katika uongozi uondolewe.

Amewaasa wanafunzi hao wanaotaka uongozi, kuwa wasikivu, welevu, wavumilivu, wafuatiliaji na wapanga mikakati.

Kamugisha amewataka vijana wanaotaka uongozi, kujitenga na matumizi ya nguvu, umaarufu na mafanikio ya haraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!