Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Marekani yataja sababu Kamala Harris kutua nchini
Habari za SiasaKimataifa

Marekani yataja sababu Kamala Harris kutua nchini

Spread the love

SERIKALI ya Marekani imesema ziara ya Makamu wa Rais wa Taifa hilo, Kamala Harris kwa nchi za Afrika ikiwamo Tanzania, ni kujadili vipaumbele vya dunia kwa sasa ambavyo ni demokrasia, uchumi shirikishi, usalama wa chakula na madhara ya Urusi kuivamia Ukraine. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Harris na msafara wake unatarajia kuanza ziara Barani Afrika kuanzia tarehe 25 Machi hadi tarehe 2 Aprili mwaka huu kwa kutembelea nchi tatu ambazo ni Tanzania, Ghana na Zambia.

Katika ziara hiyo, Makamu huyo wa Rais atakutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema pamoja na Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan.

Kamala Harris, Makamu wa Rais wa Marekani

Katika taarifa iliyotolewa leo tarehe 13 Machi 2023 na Ikulu ya Marekani, imesema, ziara hiyo inalenga kuboresha ushirikiano kati ya Marekani na nchi za Afrika kwa kuzingatia masuala ya usalama na uchumi endelevu.

Ziara hiyo ambayo pia itahusisha mazungumzo na wadau wa sekta binafsi, inalenga kujadili namna ya kuenenda na mabadiliko ya ukuaji wa uchumi kidijitali, mabadiliko ya tabianchi, uwekezaji, mazingira ya kibiashara na ujasiriamali sambamba na kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Harris ambaye ni Makamu wa Rais wa Kwanza Mwanamke katika taifa la Marekani, ujio wake unahisiwa kuwa huenda ukawa ni maandalizi ya ziara ya Rais wa Marekani, Joe Biden aliyoahidi kuifanya Afrika mwaka huu.

Itakumbukwa kuwa Aprili 2022, Rais Samia alikutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa taifa hilo, Kamala Harris jijini Washington.

Kamala Harris ambaye ni makamu wa 49 wa Marekani na yeye sasa anafanya ziara yake ya kwanza nchini Tanzania.

Marais wa Marekani ambao hadi sasa wameitembelea nchi ya Tanzania ni pamoja na Bill Clinton, George Bush, pamoja na Barack Obama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!