NAIBU Waziri wa Afya Dk. Godwin Mollel amesema kwa sasa Tanzania imepiga hatua katika kupambana na ugonjwa huo na wagonjwa wanaopatikana siyo maambukizi mapya bali ni wagonjwa zamani. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma (endelea).
Dk. Mollel ametoa kauli hiyo jana tarehe 29 Januari 2023 wakati akizungumzia kilele cha siku ya ukoma duniani ambapo pamoja na mambo mengine amesema wagonjwa wapya wa ukoma waliogundulika nchini imepungua mwaka hadi mwaka, katika miongo miwili iliyopita ambapo dunia iliongeza kasi ya kupambana na ugonjwa huo.
“Nchi yetu imeweza kuwagundua na kuwatibu wagonjwa wapya wa ukoma zadi ya 122,000 na kwa mwaka 2021 walikuwepo wagonjwa wapy 1,613.
“Tanzania tayari imefikia hatua ya awali ya kiwango cha kimataifa cha utokomezaji wa ukoma na kuwa chini ya mgonjwa mmoja kati ya watu 10,000 kwa mto mmoja kwa idadi hiyo katika nchi au katika sehemu husika.
“Hatua zinazofuata ni kutokuwa na mtoto anayeugua ukoma nchini kwa miaka mitatu, mitano na hatimaye 10 mfululizo, kwa mwaka 2021 kwa watoto waliogundulika kuugua ukoma ilifika 41 na hivyo kuonesha wazi ya kuwa mnyororo wa maambukizi bado upo na bado tuna jukumu kubwa la kufanya kukomesha kuenea kwa ugonjwa huo na kwa sasa wagonjwa wengi wanaogundulika ni wale wa zamani” ameeleza Dk. Mollel.
Hata hivyo, Dk. Mollel alitaja mikoa mbayo imekuwa na wagonjwa wengi wa ukoma kuwa ni Morogoro, Lindi, Dar es Salaam, Pwani, Mtwara, Tanga, Katavi, Dodoma, Geita, Shinyanga, Tabora na Rukwa.
Pamoja na mambo mengine Dk. Mollel amekabidhi gari la kubebea wagonjwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma kama sehemu ya kuwezesha kurahisisha utendaji kazi.
Leave a comment