Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Serikali kutaifisha mashamba ya MO Dewji
Habari Mchanganyiko

Serikali kutaifisha mashamba ya MO Dewji

Spread the love

SERIKALI imekusudia kuchukua baadhi ya mashamba yanayomilikiwa na Kampuni ya Mohammed Enterprises na kuwapa wananchi kwa kuwa kampuni hiyo imeshindwa kutimiza masharti ya uendelezaji wake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo ya serikali imekuja baada ya Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabulla kufanya ziara ya ukaguzi wa mashamba 14 yanayomilikiwa na kampuni hiyo katika wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.

Katika ziara hiyo, Waziri Mabulla alibaini kwamba Mohammed Enterprises inamiliki maeneo yenye ukubwa wa hekta 9, 418 yaliyo sawa na hekari 20,779 ambayo kampuni hiyo imechukulia mkopo kwa ajili ya kupanda mkongwe.

“Wizara yangu imejiridhisha kuwa ipo haja ya kugawa maeneo yanayomilikiwa na Mohammed Enterprises ambayo hayajaendelezwa kwa kupandwa mkonge ili wapewe wananchi ambao wana uhaba wa ardhi muda mrefu kwa sababu ya maeneo makubwa kumilikiwa na watu wachache,” amesema Waziri Mabulla.

Kwa upande wake Meneja anayesimamia mashamba hayo kutoka Mohammed Enterprises, Newalo Nyari amejitetea kwa kusema kuwa mashamba hayo waliyaendeleza na kwamba maeneo yaliyo baki waliyaacha kwa ajili ya uhifadhi wa misitu na kuwapa wananchi kwa ajili ya kupanda mazao yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!