Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Mnangawa achekelea Uchaguzi Zimbabwe
Kimataifa

Rais Mnangawa achekelea Uchaguzi Zimbabwe

Spread the love

WAKATI kura zikiendelea kuhesabiwa katika uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika, Rais wa nchi hiyo Emmerson Mnangawa ambaye ni mmoja wa wagombea ameonesha kuwa, ana matumaini makubwa ya kushinda baada ya kuonesha hisia zake kwenye ukurasa wake wa twitter.

Ujumbe huo unaelezea furaha yake baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wawakilishi wake waliopo kwenye vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo amesema, yeye na wafuasi wake watasubiri mpaka matokeo rasmi yatangazwe kama ilivyo taratibu za sheria za nchi hiyo.

” Good morning Zimbabwe. I am delighted by the high turnout and citizen engagement so far. The information from our reps on the ground is extremely positive! Waiting patiently for official results as per the constitution”

Rais Mnangagwa alichukua mamlaka baada ya urais baada ya jeshi kuingilia kati mnamo Novemba 15 mwaka jana kufuatia mgogoro wa kumrithi mhasisi wa nchi hiyo Robert Mugabe.

Huku matokeo ya awali yakitarajiwa kutangazwa muda wote kuanzia sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!