Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serengeti yashinda tuzo hifadhi bora Afrika mara ya nne mfululizo
Habari Mchanganyiko

Serengeti yashinda tuzo hifadhi bora Afrika mara ya nne mfululizo

Serengeti
Spread the love

HIFADHI ya Taifa ya Serengeti imeshinda tuzo ya Hifadhi bora zaidi barani Afrika 2022 ikiwa ni mara ya nne  mfululizo baada ya kushinda tena mwaka 2019, 2020 na 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hifadhi hiyo imezibwaga hifadhi za Central Kalahari ya Botswana, Kruger National Park ya Afrika Kusini, Kidepo Valley Nationa Park (Uganda), Etosha National park (Namibia) na Masai Mara National Reserve ya Kenya.

Tuzo hizo zilizoanzishwa mwaka 1993 kutambua na kutunza ubora wa urithi huo wa rasilimali za hifadhi, zinatolewa World Travel Award (WTA) na zinatambulika kimataifa.

Serengeti ni miongoni mwa hifadhi 19 zilizopo chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ambazo zimetapakaa  katika kanda za Kusini, Kaskazini, Mashariki na Magharibi.

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti iliyopo mkoani Mara ipo kanda ya Kaskazini ikiwa maarufu kwa tukio la kipekee la kuhama kwa mamilioni ya nyumbu ambayo huvuka mto Mara kila mwaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!