RAIS Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku nne mkoani Kigoma, kuanzia tarehe 16 hadi 19, Oktoba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu ziara hiyo, leo tarehe 11 Oktoba, 2022 Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amesema ziara ya Rais Samia itaanzia wilayani Kakonko.
Amesema akiwa mkoani Kigoma, pamoja na mambo mengine Rais Samia atafungua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Aidha, Andengenye amewataka wakazi wa wilaya za mkoa wa Kigoma ambazo Rais atapitia zikiwemo za Kakonko, Kibondo Kasulu, Buhigwe na Kigoma kujitokeza kwa wingi kumpokea kiongozi huyo.
Ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan mkoani Kigoma ni ya kwanza tangu aingie madarakani mwezi Machi mwaka 2021.
Leave a comment