Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia: Tunashukuru IMF, tumejadiliana wakatuelewa
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia: Tunashukuru IMF, tumejadiliana wakatuelewa

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amelishuruku Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa kuielewa Serikali ya Tanzania na kuridhia itumie fedha za maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 kwa namna inatakavyoona inafaa. Anaripoti Mwandishi wetu (endelea)

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 10 Oktoba, 2021 jijini Dodoma wakati akizindua kampeni ya maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 ambao umetokana na mkopo nafuu wa Sh trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika hilo la IMF.

Amesema mpango uliozinduliwa leo utagharimu fedha nyingi katika miradi mbalimbali itakayotekelezwa kwa nchi nzima yaani Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema upatikanaji wa fedha ulikuwa na ‘mbinumbinu’, lakini anashukuru IMF kwa kuelewana  na Serikali ya Tanzania na kujadiliana kisha wakaleta timu yao ya watalaam ambayo iliendelea kujadiliana na Tanzania.

“Wenzetu waliopata pesa hizi wamezielekeza mzigo wote kwenye manunuzi ya chanjo na vitu vingine vya kujikinga na Corona, kwa upande wetu tukasema hapana.

“Ili tuweze kukabiliana vema na Corona lazima tuwe na maji, tupunguze masafa ya wanafunzi kubana, lazima tuwe vituo vya afya vingi vitakavyotoa huduma zipasavyo kuanzia ngazi ya wilaya hadi chini ili Corona ikipiga hadi kule chini kuwepo na vituo vya afya. Tunashukuru walituelewa wakaridhia fedha hizi tuzitumie kama sisi tulivyoona inafaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!