RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Dk. John Kedi Mduma kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, imesema uteuzi wa Dk. Mduma umeanza leo Jumamosi, tarehe 24 Aprili 2021.
Amesema, Dk. Mduma ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.
Ninalipenda sana gazeti letu la mwanainchi Lina habari za ukweli sana, na linatuelimisha sana, hongereni sana,