Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Simba yaishusha Yanga kileleni
Michezo

Simba yaishusha Yanga kileleni

Spread the love

Bao la dakika ya 28 lililofungwa na Mohammed Hussein kwenye mchezo dhidi ya Gwambina lilitosha kuipeleka Simba kileleni kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kuishusha Yanga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Mchezo huo ulipigwa hii leo kwenye Uwanja wa Gwambina uliopo Misumbwi mkoani Mwanza.

Mechi hiyo ilikuwa yenye mvuto wa aina yake kutokana timu zote kucheza na taadhari kubwa kutokana na ubora wa vikosi vya timu zote mbili.

Iliwachukua Simba dakika 28 kwa Simba kuandika bao hilo la kwanza na la ushindi lililofungwa kwa shuti kali na beki wa kushoto wa Simba Mohamed Hussen na kudumu mpaka dakika 90 ya mchezo.

Matokeo ya mchezo huo yaliifanya Simba kuishusha Yanga kwa tofauti ya alama moja na Simba akiwa nyuma kwa michezo miwili.

Simba inafikisha pointi 58, wakiwa na michezo 24 huku Yanga iliyoongoza Ligi hiyo muda mrefu, imepolomoka mpaka nafasi ya pili wakiwa na pointi 57 na michezo 26.

Yanga itashuka dimbani kesho kupambana na Azam FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu utakaopigwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!