Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aeleza Kamala alivyopata Corona, “mimi mzima”
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia aeleza Kamala alivyopata Corona, “mimi mzima”

Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefafanua kuwa baada ya kukutana Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris, alipokuwa kwenye ziara nchini humo, Kamala alipimwa na majibu kutoka kuwa hana maambukizi ya virusi vya Corona.

Amesema wiki moja baada ya kukutana na makamu huyo wa Rais, aligundulika kuambukizwa virusi hivyo vinavyosababisha ugonjwa wa Covid- 19 hii ikiwa ni baada ya kiongozi huyo wa Marekani kwenye ziara zake za kikazi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Mei, 2022  jijini Arusha katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani.

Ametolea mfano namna alivyochorwa kikatuni kuelezea kuwa amemuambukiza Virusi vya Corona Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris.

“Nimeona kwenye mitandao ya kijamii… Rais wenu kaenda kuonana na Makamu wa Rais wa Marekani, baada ya wiki yule bibi yupo positive COVID-19, mimi mzima!

“Mtanzania kaweka kikatuni katia mshale unatoka kwangu unakwenda kwa Kamala kwamba mimi nimempa COVID-19 lakini alipimwa baada ya mimi kuondoka yupo negative, kaenda ziara karudi ndio yupo positive, ulizeni… mnajiandikia tu, miye nina ngozi ngumu, andikeni,” amesema.

Rais Samia alielekea nchini Marekani Aprili 13 hadi 28 mwaka huu kwenda kuzindua filamu inayotangaza utalii wa Tanzania maarufu kama ‘Royal tour’

Aidha, ametoa wito kwa vyombo vya habari kuelimisha umma kuhusu matumizi bora ya mitandao ya kijamii hasa ikizingatiwa wapo wengine wanaitumia vibaya kwa kuweka picha na video zisizo na maadili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!