Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Museveni amteua mwanaye kuwa mkuu wa majeshi
Habari MchanganyikoKimataifa

Rais Museveni amteua mwanaye kuwa mkuu wa majeshi

Spread the love

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amemteua mtoto wake wa kiume Jenerali Muhoozi Kainerugaba kuwa mkuu wa majeshiya nchi hiyo uteuzi ambao umetajwa kudhihirisha wazi kuwa huenda kiongozi huyo anamuandaa mtoto wake kumrithi atakapoachia madaraka. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Muhoozi Kainerugaba anachukua nafasi ya Jenerali Wilson Mbasu Mbadi ambaye ameteuliwa kuwa waziri wa biashara katika mabadiliko mapya ya baraza la mawaziri yaliyotangazwa jana jioni.

Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi, washauri wake wawili wa karibu pia wamepewa nyadhifa za uwaziri na kuchochea uvumi kwamba Rais Museveni anaunga mkono shughuli za kisiasa Muhoozi Kainerugaba.

Mtoto huyo wa kwanza wa rais amekuwa akifanya mikutano ya hadhara kote nchini, hatua ambayo inakwenda kinyume na sheria inayowazuia maafisa wa jeshi kujihusisha na siasa.

Kainerugaba hata hivyo amejitetea kwa kueleza kuwa shughuli zake – ikiwa ni pamoja na uzinduzi wa hivi karibuni wa kundi la uanaharakati la Patriotic League of Uganda – aliyesema kundi hilo linanuia kuhimiza kujenga uzalendo miongoni mwa Waganda.

Museveni ambaye kwa mara ya kwanza alichukua madaraka kwa nguvu mnamo mwaka 1986, na kuchaguliwa mara sita, hajaeleza ni lini atakapostaafu.

Kiongozi huyo pia hana mpinzani ndani ya chama tawala cha NRM huku wengi wakiamini kuwa jeshi litakuwa na sauti katika kuchagua mrithi wake.

Kulingana na wachambuzi, washirika wa Kainerugaba wameteuliwa kimkakati kwenye nafasi za juu za idara ya usalama. Uganda itaanda uchaguzi mkuu ujao mwaka 2026.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!