Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwenyekiti UVCCM auawa kwenye fumanizi
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwenyekiti UVCCM auawa kwenye fumanizi

Spread the love

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana  wa CCM (UVCCM) kata ya Kaselya Wilaya ya Iramba  mkoani Singida, Ramadhani Hamisi (30) ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali tumboni.

Kadhia hiyo ilimkuta Ijumaa iliyopita usiku katika kitongoji cha Musisi karibu na Kaselya Mabandani ikidaiwa alikutwa akiwa na mke wa Ally thumani. Anaripoti Thomasi Kiani, Singida…(endelea).

Habari zinadai kuwa Hamisi alikuwa na mahusiano  ya kimapenzi  na mke  wa Athumani kwa   muda mrefu  na walishakutwa  mara  nyingi  na  kuonywa  na mwenye mali aache  mchezo huo. Inadaiwa siku hiyo ya Ijumaa Athumani aliwakuta nyumbani kwake.

Kwa mujibu wa habari zilizotolewa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kaselya, Wazzael Maija tukio hilo lilitokea saa 4 usiku katika kitongoji cha Musisi.

Habari zinadai kuwa baada ya  Athumani kuwafuma, ugomvi uliibuka na kufukuzana gizani  na kupotezana njiani lakini Athumani alimvizia  nyumbani  na bila kujua muda Ramadhani akamshambulia.

Inadaiwa alimchoma tumboni  na kitu chenye  ncha  kali upande  wa kulia wa tumbo na utumbo kuchomoza nje na damu  nyingi kuvuja na hatimaye kuanguka.

Baada ya kubaini hivyo, Athumani alienda kwa mzazi wa Ramadhani, Ally  Hamisi na kumwambia akamuone  mwanae  anakufa.

”Mimi tayari kazi nimeimaliza nimemkuta  mwanao anamchezea  mke  wangu” anadaiwa kumwambia mzee huyo na kuondoka.

Habari zinadai Hamisi alipotoka nje alimkuta mwanaye hajiwezi  damu ikimvuja tumboni akachanganyikiwa, lakini Ramadhani akiwa  bado anafahamu kidogo  akamwambia  baba yake, “nikifa  nimeuawa  na Ali, amenichoma  na  kisu  akakimbia.”

Mzee Hamisi alipiga yowe  majirani walifika na  kuamua  Ali  na  mkewe  wakamatwe  wawekwe  chini  ya ulinzi  huku Ramadhani  akikimbizwa Hospitali ya mkoa wa Singida  kwa matibabu.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Msisi Haruna Hamisi amesema majeruhi alipelekwa usiku huohuo Hospitali ya Singida  kwa  gari baada  ya wananchi  kumsaidia  huduma za kwanza  kwa kumfunga  nguo jeraha  hilo.

Amesema waganga  wa Hospitali  hiyo  walijitahidi kuokoa  maisha yake  lakini  haikuwezekana  kwani muda mfupi baadae  alifariki  dunia  kwa kutokwa  na damu  nyingi  hasa ikizingatiwa jeraha  lilikuwa  pabaya

Aidha, Mwenyekiti  Haruna  Hamisi  amesema  watu  waliotumwa kumthibiti Athumani  na Mke  wake  hawakuwakuta,  wote   walishaondoka  usiku  uleule  na hawajulikani walikokwenda  hadi sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!