Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 37 anakabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya mpenzi wake aliyefahamika kwa jina moja la Milca (48) kufariki dunia wakati wakifanya mapenzi kichakani eneo la Mbita katika Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Kwa mujibu wa mtandao wa TUKO, tukio hilo limetokea Jumapili jioni tarehe 19 Machi 19 2023 baada ya wapenzi hao waliokuwa wanarejea nyumbani kuamua kuingia kwenye kichaka eneo la Got Rateng kwa ajili ya kufanya kitendo hicho walipokuwa wametoka kunywa pombe.
Chifu wa eneo hilo Bernard Ouma amesema kuwa wawili hao awali walikuwa wameonywa wasishiriki tendo wakiwa wamelewa lakini hawakutii.
Amesema mshtakiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini humo baada ya kukiri chanzo cha kifo hicho.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa mwanaume huyo amemrithi Milca baada ya kifo cha mume wake kama ilivyo utamadumi wa wakazi wa eneo hilo, ambapo mwanamke anaruhusiwa kurithiwa pale mumewe anapofariki.
“Baada ya kifo cha Milca alijaribu kuuzika mwili wake na ndipo tukamkamata mshtakiwa.
“Kuna wakati niliwaita na kuwaonya kuhusu kufanya mapenzi sehemu zisizo na staha hasa baada ya kunywa pombe, waliendelea na ninafikiri hilo linaweza kuwa chanzo cha maafa haya,” amesema Chifu Ouma.
Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Homa Bay huku uchunguzi zaidi ukiendelea.
1
-5) OR 516=(SELECT 516 FROM PG_SLEEP(15))–
-1)) OR 968=(SELECT 968 FROM PG_SLEEP(15))–
wSjaLxjC’)) OR 761=(SELECT 761 FROM PG_SLEEP(15))–
1′”
@@ujG6L
KWA AJILI YA MASHINDANO YA MTU WA KWANZA KUWAHI PATIKANA DUNIANI – UKIONA VIPI TUMA KWENYE ANUANI HII
H.E Ambassador
Dr. Emmanuel John Nchimbi
The Embassy of the United Republic of Tanzania
10 ANAS Ibn Malek Street,
Mohandessin,
Cairo, Egypt
Postal Code: 12411