Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwanamke afariki akifanya mapenzi kichakani
Habari Mchanganyiko

Mwanamke afariki akifanya mapenzi kichakani

Spread the love

 

Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 37 anakabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya mpenzi wake aliyefahamika kwa jina moja la Milca (48) kufariki dunia wakati wakifanya mapenzi kichakani eneo la Mbita katika Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa TUKO, tukio hilo limetokea Jumapili jioni tarehe 19 Machi 19 2023 baada ya wapenzi hao waliokuwa wanarejea nyumbani kuamua kuingia kwenye kichaka eneo la Got Rateng kwa ajili ya kufanya kitendo hicho walipokuwa wametoka kunywa pombe.

Chifu wa eneo hilo Bernard Ouma amesema kuwa wawili hao awali walikuwa wameonywa wasishiriki tendo wakiwa wamelewa lakini hawakutii.

Amesema mshtakiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini humo baada ya kukiri chanzo cha kifo hicho.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa mwanaume huyo amemrithi Milca baada ya kifo cha mume wake kama ilivyo utamadumi wa wakazi wa eneo hilo, ambapo mwanamke anaruhusiwa kurithiwa pale mumewe anapofariki.

“Baada ya kifo cha Milca alijaribu kuuzika mwili wake na ndipo tukamkamata mshtakiwa.

“Kuna wakati niliwaita na kuwaonya kuhusu kufanya mapenzi sehemu zisizo na staha hasa baada ya kunywa pombe, waliendelea na ninafikiri hilo linaweza kuwa chanzo cha maafa haya,” amesema Chifu Ouma.

Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Homa Bay huku uchunguzi zaidi ukiendelea.

7 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!