Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwabukusi, Mdude nao waachiwa kwa dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Mwabukusi, Mdude nao waachiwa kwa dhamana

Spread the love

 

HATIMAYE Wakili, Boniphace Mwabukusi na Kada wa Chasema, Mpaluka Saidi Nyangali maarufu kama ‘Mdude’ nao wameachiwa huru na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya baada ya kutimiza masharti ya dhamana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Wawili hao wameachiwa huru jioni leo Ijumaa ikiwa ni saa chache baada ya Dk. Willibroad Slaa naye kuachiwa huru mchana na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Wakili wa wawili hao, Philip Mwakilima amesema watuhumiwa hao awali waliandikishwa maelezo kuwa watuhumiwa wa makosa ya uhaini lakini sasa wameachiwa kwa tuhuma za uchochezi.

“Leo asubuhi tulipewa taarifa kwamba tuwajulishe ndugu wa wateja wetu walete wadhamini na sasa wamedhaminiwa wakituhumiwa na kosa la uchochezi. Kila mtuhumiwa alitakiwa awe na wadhamini wawili wawe na mali isiyohamishika yenye thamani isiyo chini ya Sh 10 milioni pamoja na barua kutoka serikali za mitaa,” amesema.

Naye Wakili Mwabukusi akizungumza baada ya kuachiwa huru mbali na kushukuru Watanzania amesema Mungu amewatumia kama sauti ili wawe nje leo kwani lengo la mashtaka hayo ya uhaini ni kuwaua kama ilivyo adhabu yake.

 

“Kwa hiyo walitaka tunyongwe kwani ndio adhabu ya shtaka hilo. Tunaamini Mungu amewatumia kupaza sauti tunawashukuru sana, tuwahakikishie tutatoa maelezo yetu na muelekeo wetu,” amesema na kuongeza;

“Ila watambue kwamba hatujayumbishwa hatujatetereshwa wala kubabaishwa katika kutimiza wajibu wetu kama watanzania, naamini ndege ikipaa huwa haina reverse, kwa hiyo msimamo upo palepale kama tulivyomaliza hatua yetu ya mwisho.”

Amesema licha ya kwamba wameachiwa, ni kwamba walikuwa kizuizini jambo ambalo ni kinyume cha katiba.

“Niko hapa kwa sababu ya solidarity ya ndani na nje ya nchi, na vyombo vya habari… ninawashukuru sana ila kwa leo kwa sababu nina complication kidogo za afya, mwili haupo stable sana nitasema bayana what next,” amesema.

Kwa upande wake Mdude amesema baada ya kutoka kizuizini walipokuwa wamewekwa kwa siku tisa, watawasiliana na mwenzao Dk Slaa ili waanzie walipoishia.

“Tunaanzia tulipoishia ngoma hairudi nyuma. Tutazungumza na waandishi wa habari kwamba tutaendaje mbele kwani haturudi. Maandamano sio kosa la uhaini halijakatazwa na sheria yoyote ya nchi… mkiniweka humo ndani mnanitekenya, polisi ni sebule, gerezani ni chumbani kwangu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!