Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mwabukusi, Mdude nao waachiwa kwa dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Mwabukusi, Mdude nao waachiwa kwa dhamana

Spread the love

 

HATIMAYE Wakili, Boniphace Mwabukusi na Kada wa Chasema, Mpaluka Saidi Nyangali maarufu kama ‘Mdude’ nao wameachiwa huru na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya baada ya kutimiza masharti ya dhamana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Wawili hao wameachiwa huru jioni leo Ijumaa ikiwa ni saa chache baada ya Dk. Willibroad Slaa naye kuachiwa huru mchana na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Wakili wa wawili hao, Philip Mwakilima amesema watuhumiwa hao awali waliandikishwa maelezo kuwa watuhumiwa wa makosa ya uhaini lakini sasa wameachiwa kwa tuhuma za uchochezi.

“Leo asubuhi tulipewa taarifa kwamba tuwajulishe ndugu wa wateja wetu walete wadhamini na sasa wamedhaminiwa wakituhumiwa na kosa la uchochezi. Kila mtuhumiwa alitakiwa awe na wadhamini wawili wawe na mali isiyohamishika yenye thamani isiyo chini ya Sh 10 milioni pamoja na barua kutoka serikali za mitaa,” amesema.

Naye Wakili Mwabukusi akizungumza baada ya kuachiwa huru mbali na kushukuru Watanzania amesema Mungu amewatumia kama sauti ili wawe nje leo kwani lengo la mashtaka hayo ya uhaini ni kuwaua kama ilivyo adhabu yake.

 

“Kwa hiyo walitaka tunyongwe kwani ndio adhabu ya shtaka hilo. Tunaamini Mungu amewatumia kupaza sauti tunawashukuru sana, tuwahakikishie tutatoa maelezo yetu na muelekeo wetu,” amesema na kuongeza;

“Ila watambue kwamba hatujayumbishwa hatujatetereshwa wala kubabaishwa katika kutimiza wajibu wetu kama watanzania, naamini ndege ikipaa huwa haina reverse, kwa hiyo msimamo upo palepale kama tulivyomaliza hatua yetu ya mwisho.”

Amesema licha ya kwamba wameachiwa, ni kwamba walikuwa kizuizini jambo ambalo ni kinyume cha katiba.

“Niko hapa kwa sababu ya solidarity ya ndani na nje ya nchi, na vyombo vya habari… ninawashukuru sana ila kwa leo kwa sababu nina complication kidogo za afya, mwili haupo stable sana nitasema bayana what next,” amesema.

Kwa upande wake Mdude amesema baada ya kutoka kizuizini walipokuwa wamewekwa kwa siku tisa, watawasiliana na mwenzao Dk Slaa ili waanzie walipoishia.

“Tunaanzia tulipoishia ngoma hairudi nyuma. Tutazungumza na waandishi wa habari kwamba tutaendaje mbele kwani haturudi. Maandamano sio kosa la uhaini halijakatazwa na sheria yoyote ya nchi… mkiniweka humo ndani mnanitekenya, polisi ni sebule, gerezani ni chumbani kwangu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!