Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtulia: Yawezekana sijaiva kimkakati CCM lakini sijashindwa
Habari za Siasa

Mtulia: Yawezekana sijaiva kimkakati CCM lakini sijashindwa

Maulid Mtulia
Spread the love

MAULID Mtulia, mbunge anayemaliza muda wake wa Kinondoni jijini Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekubali matokeo na kukiri yeye bado ni mchanga kwenye siasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)

Amesema yeye hajaiva kimikakati tofauti na watia nia wenzake 79 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.

Mtulia ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura za maoni jimbo la Kinondoni.

Katika matokeo hayo, Mtulia alipata kura 11 kati ya kura 404 zilizopigwa katika mkutano huo, huku Abbas Tarimba akiongoza kwa kupata kura 171 akifuatiwa na Iddi Azan mwenye kura 77.

Katika uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba 2015, Mtulia alishinda akiwa Chama Cha Wananchi (CUF) lakini tarehe 2 Desemba 2017 alitangaza kujizulu nafasi hiyo na kuhamia CCM kuunga juhudi zinazofanywa na Serikali chini ya Rais John Magufuli.

Akizungumzia matokeo hayo, Mtulia amesema, “mimi bado ni mchanga kwenye siasa za chama cha mapinduzi ndio kwanza nina miaka miwili, yawezekana sijaiva kimikakati kama wenzangu walivyoiva.”

Aidha Mtulia amesema zoezi la kupiga kura lilienda vizuri na hakuna mtu mwenye manung’uniko ila kwa sasa wanakiachia chama kiendelee na mchakato wake.

“Huu ni mchakato na usiseme nimeshindwa, hizi ni kura za maoni na mchakato wa ndani ya chama bado unaendelea, kwa hiyo swala la kupata au kukosa nafasi sio wakati wake hivi sasa, tuaachia vikao vinaendelea na mchakato wa kumnpata mgombea wetu wa chama cha mapinduzi” amesema Mtulia.

2 Comments

  • Well done & written.
    I’ve just strted writing in the past few weeks and observed that lot
    of people merely rework old ideas but add very little of benefit.
    It’s good too read aan informative article of some actual value to me,
    as a reader.
    It’s going down on the list of things I need to replicate as
    a new blogger. Audience engagement and material value are king.

    Some terrific ideas; you have certainly managed to get on my list of blogs to follow!

    Carry on the good work!
    Well done,
    Berenice

  • View the Best Movie of All Time
    What video do you want in order to watch today?
    Sniper movies may be required on your list.
    This is the most fun shooting struggle, where every sniper actions is always interesting
    to watch.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!