Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtanzania aomba Ziwa Victoria libadilishwe jina
Habari Mchanganyiko

Mtanzania aomba Ziwa Victoria libadilishwe jina

Spread the love

DAKTARI Abdullah Hasnuu Makame, leo tarehe 6 Desemba 2019, amefikisha azimio la kubadilisha jina la Ziwa Victoria, katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Katika azimio lake hilo, Dk. Makame amelitaka Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kubadili jina la ziwa hilo, ili lipewe jina la Ki-Afrika.

Akikazia hoja yake hiyo, Dk. Makame amesema kubadilishwa kwa jina la Ziwa Victoria, itakuwa hatua muhimu katika kuzitambulisha nchi za Afrika, kwamba ziko huru kutoka kwa utawala wa kikoloni.

“Haya ni matukio ya uhuru, mabadiliko ya jina ni hatua inayoibua mahitaji ya kujitambulisha sisi kama wa Afrika, walio huru kutoka utawala wa kikoloni,” ameandika Dk. Makame katika ukurasa wake wa Twitter, leo tarehe 6 Desemba 2019.

Ziwa Victoria ni ziwa kubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambapo linapaka na nchi ya Tanzania, Kenya na Uganda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!