Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili wa Vyama vya Siasa ‘akaangwa’ bungeni
Habari za Siasa

Msajili wa Vyama vya Siasa ‘akaangwa’ bungeni

Spread the love

JAJI Francis Katabazi Mutungi, ameonywa kutojilimbikizia madaraka na kutaka kujiwekea kinga ya kutoshitakiwa mahakamani wakati yeye amebeba roho ya umma. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Onyo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Vicenti Mashinji, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, mjini Dodoma.

Taarifa kutoka ndani ya kamati hiyo, zinaeleza kuwa chama hicho kimedai kuwa mapendekezo yaliyomo kwenye baadhi ya vifungu vya muswada, “yanampa Msajili mamlaka ya Kiungu.”

“Hapa kuna hila. Hakuna hiyo nia njema inayotajwa. Ndio maana msajili anahofia kupelekwa mahakamani. Kama angekuwa anaongozwa na dhamira njema, hili lisingekuwapo. Ndio maana anataka kinga. Nadhani kuna jambo baya ambalo analitaka kulifanya,” ameeleza Dk. Mashinji.

Amesema, “ni bahati mbaya sana, kwamba sheria hii inasimamiwa na msajili ambaye ni jaji wa Mahakama Kuu. Hatua ya Jaji kuogopa mahakama, kunathibitisha kuwa kuna nia ovu.”

Tangu kuwasilishwa bungeni muswada wa sheria ya vyama vya siasa, kumeibuka malumbano makali kati ya viongozi wa vyama vya upinzani na wale wanaotoka chama tawala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!