Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili wa Vyama vya Siasa ‘akaangwa’ bungeni
Habari za Siasa

Msajili wa Vyama vya Siasa ‘akaangwa’ bungeni

Spread the love

JAJI Francis Katabazi Mutungi, ameonywa kutojilimbikizia madaraka na kutaka kujiwekea kinga ya kutoshitakiwa mahakamani wakati yeye amebeba roho ya umma. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Onyo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Vicenti Mashinji, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, mjini Dodoma.

Taarifa kutoka ndani ya kamati hiyo, zinaeleza kuwa chama hicho kimedai kuwa mapendekezo yaliyomo kwenye baadhi ya vifungu vya muswada, “yanampa Msajili mamlaka ya Kiungu.”

“Hapa kuna hila. Hakuna hiyo nia njema inayotajwa. Ndio maana msajili anahofia kupelekwa mahakamani. Kama angekuwa anaongozwa na dhamira njema, hili lisingekuwapo. Ndio maana anataka kinga. Nadhani kuna jambo baya ambalo analitaka kulifanya,” ameeleza Dk. Mashinji.

Amesema, “ni bahati mbaya sana, kwamba sheria hii inasimamiwa na msajili ambaye ni jaji wa Mahakama Kuu. Hatua ya Jaji kuogopa mahakama, kunathibitisha kuwa kuna nia ovu.”

Tangu kuwasilishwa bungeni muswada wa sheria ya vyama vya siasa, kumeibuka malumbano makali kati ya viongozi wa vyama vya upinzani na wale wanaotoka chama tawala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!