WADAU wa maliasili wamekutana kujadili namna ya kudhibiti mianya ya upitishaji miamala ya fedha kwa njia mitindao na benki inayolenga kufadhili biashara ya maliasili na ujangili nchini. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).
Mjadala huo unaoratibiwa na Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) iliwakutanisha wadau wa mitandao pamoja na benki ulioanza leo tarehe 7 na kutamatishwa kesho tarehe 8 Desemba 2023 jijini Dar es Saalam.
Godfrey Mondi Meneja Miradi wa TPSF amesema kuwa warsha hiyo ya siku mbili imelenga kutoa elimu kwa watoa huduma za kifedha kwa njia za benki na mitandao ya simu ili kudhibiti viashiria vya miamala ya fedha inayolengwa kufanyiwa biashara haramu ya kusafirisha Rasimali.
“Tunawajengea uwezo watu wa mitandao na benki ili kudhibiti miamala inayopita kwenye mitandao na benki inayoweza kuendesha biashara harama,” amesema Mondi.
Amesema kuwa mradi huo unaofadhiliwa na watu wa Marekani (USAID) unaitwa ‘Tuhifadhi Maliasili’ unalenga kupambana na ujangili.
Amesema kuwa miamala inayofanywa kwa kujirudia kwenye maeneo ya maliasili ni ya kuijengea shaka.
Leave a comment