Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mgomo wa mabasi wanukia Tanzania
Habari Mchanganyiko

Mgomo wa mabasi wanukia Tanzania

Mabasi yakiwa kituo cha mabasi Mbezi
Spread the love

 

CHAMA cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), kimetoa siku tatu kwa mamlaka zinazohusika na mfumo wa mashine za kukatia tiketi kwa njia ya mtandao (POS), kutatua changamoto zinazoukabili “lasivyo hatuteweza tena kutoa huduma.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taboa wanalalamikia mfumo huo wakidai si rafiki na kuitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (Latra), kuachana na mfumo huo kwani unawasababishia hasara.

Uamuzi huo, wameutoa leo Jumamosi tarehe 6 Machi 2021, katika kikao cha dharura cha wamiliki wa mabasi kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

“Leo tarehe 6 Machi 2021, Taboa tumefanya mkutano mkuu wa dharura juu ya changamoto zinazotokana na mfumo huu ambao si rafiki wa POS, kumekuwa na faini za kila leo kutoka Latra bila kujali changamoto za mfumo.”

“Latra imekuwa ikifungia magari ya wamiliki wanaoshindwa kutumia mfumo bila kutatua changamoto za mfumo husika,” amesema mwakili wa wamiliki hao, Max Komba

“Hivyo basi, kwa kauli moja wanachama wameazimia kuwa, kwa kuwa mfumo wa kielekoniki si rafiki ni kandamizi, wasafirisgaji watashindwa kutoa huduma na tunatoa siku tatu kwa mamlaka kutatua changamoto,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!