Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mchungaji Kenya ahukumiwa miaka 75 jela
Habari Mchanganyiko

Mchungaji Kenya ahukumiwa miaka 75 jela

Spread the love

ASKOFU katika kaunti ya Kisumu nchini Kenya, Joseph Agutu amehukumiwa kifungo cha miaka 75 jela baada ya mahakama kumkukuta na hatia ya kuwabaka watoto wa kike watatu, huku mmoja kati yao akimuambikiza Virusi vya Ukimwi(VVU). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hukumu hiyo ilitolewa jana tarehe 18 Desemba 2018 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Pauline Mbulika baada ya ushahidi uliotolewa na mmoja kati ya mashahidi katika kesi hiyo, kuthibitisha kwamba askofu huyo alifanya ngono zembe zaidi ya mara tano kwa watoto hao.

Agutu alihukumiwa kifungo hicho na mahakama kutokana na makosa manne yaliyokuwa yakimkabili, ambapo alitenda katika nyakati tofauti kwenye kipindi cha mwezi Aprili na Julai mwaka 2016 katika eneo la Kachok.

Katika makosa hayo, Askofu huyo alishtakiwa kwa kumuambukiza VVU kwa makusudi mtoto mmoja. Agutu amefungwa miaka 20 jela kwa kila kosa katika makosa matatu, wakati kosa la nne akifungwa miaka 15.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!