Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mchimbaji mdogo anunua mtambo wa milioni 200, amshukuru Samia
Habari Mchanganyiko

Mchimbaji mdogo anunua mtambo wa milioni 200, amshukuru Samia

Spread the love

JITIHADA za Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwainua wachimbaji wadogo wa madini, zimeendelea kuonekana baada ya Mchimbaji mdogo wa Dhahabu kutoka Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Marwa Maginga kununua mtambo wa uchimbaji wa dhahabu aina ya Katapila kwa gharama ya zaidi ya Sh milioni 200. Anaripoti Paul Kayanda, Mara… (endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 4 Septemba, 2022 mkoani Mara katika maonesho ya Mara International Business Expo 2022 yaliyoandaliwa na Chemba ya biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania Mkoa wa Mara.

Marwa Maginga mwenye tisheti nyeupe akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine katika Mkoa wa Mara.

Maonesho hayo yanalenga kuutangaza mkoa huo kupitia vivutio na fursa kibiashata zilizopo katika eneo hilo kwa Afrika Mashariki.

Akizungumia ununuzi wa mtambo huo, Mchimbaji huyo alisema hatua aliyoipiga inatokana na ari ya Rais Samia kuendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa wachimbaji wadogo.

Alisema Rais Samia amewatengenezea fusa mbalimbali na kwamba kadri siku zinavyozidi kusonga sekta ya uchimbaji mdogo inazidi kuthaminika na wahusika kutumia mwanya huo kuendelea kukuza mitaji yao.

“Sisi wachimbaji wadogo kwa kweli tunaomba Rais wetu mpendwa aendelee kutushika mkono kwa kuendelea kututengenezea mazingira mazuri zaidi ili ifikie wakati nasisi tumudu uchimbaji wa kati na uchimbaji mkubwa,” alisema.

Aidha, Msemaji wa kampuni ya Meta Plant and EQuepment Tanzania Ltd., Edwin Ruangisa ambayo imemuuia mtambo huo alisema; “Kifaa hicho tulichomuuzia mteja wetu kitamsaidia kwa shughuli mbalimbali na siyo uchimbaji wa madini ya dhahabu peke yake, bali kifaa hicho kitamwingizia faida kwa shughuli zingine za ujenzi wa miundo mbinu na majengo.”

Naye Mwenyekiti wa chemba ya biashara mkoa wa Mara, Boniphace Ndengo aliahidi kuendelea kuisaidia serikali kunyanyua uchumi kupitia sekta ya madini kwa kuwashika mkono wachimbaji wadogo.

“Nami nimpongeza Rais Samia  kutusaidia sisi wawekezaji wakubwa pamoja na wajasiriamali kupata uthubutu mkubwa kwenda kwenye sekta kubwa kama hizi… hali hiyo inakwenda kujenga ushindani na makampuni makubwa,” alisema Ndengo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!