MCHEZAJI na kapteni wa timu ya vijana ya Singida Big Star (U17), Mohammed Banda leo tarehe 19 Januari, 2023 amefariki dunia baada ya kugongana kichwani na mchezaji mwenzake wakiwa mazoezini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na uongozi wa Klabu hiyo kupitia akaunti yao ya mtandao wa Instagram, Banda alipoteza maisha alipofikishwa Hospitali ya Mkoa wa Singida baada ya kugongana kichwani na mchezaji mwenzake wakiwa mazoezini katika Uwanja wa Magereza, Singida.
“Tunathibitisha kutokea kwa kifo cha aliyekuwa mchezaji na kapteni wa timu yetu ya vijana (U17), Mohammed Banda, kilichotokea leo asubuhi Januari 19, 2023.
“Tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu mzito,” imesema taarifa hiyo.
Leave a comment