MCHUNGAJI wa Kanisa la Mlima wa Moto (Mikocheni B Assemblies of God), amefariki dunia alfajiri ya leo tarehe 20 Aprili 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa ya kifo hicho imethibitishwa na miongoni mwa Askofu wa Kanisa hilo, Joachim Kimanza.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa familia yake, Mama Rwakatale alikuwa anasumbuliwa na presha.
Hadi umauti unamfika, Mama Rwakatale alikuwa mbunge viti maalumu kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE kwa taarifa zaidi.
Leave a comment