Saturday , 27 April 2024
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe avamiwa

Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, yupo kwenye wakati mgumu jimboni kwake Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea).

Akiwa kwenye mkutano jana tarehe 3 Machi 2020, alivamiwa na vijana walioandaliwa kuvuruga mkutano wake, ikiwa ni hatua za kuzima kile kilichoitwa dhamira ya kugombea tena ubunge kwenye jimbo hilo.

Mkutano huo ulikuwa ukifanyika katika Kijiji cha Kikafu Chini, Kata ya Weruweru, ambapo kikundi cha vijana wa kike na kiume liliibuka na kuanza kufanya vurugu.

Akiwa jukwaani anahutubia, ziliibuka kelele za vijana hao na kusababisha kunyamaza kwa muda, vijana hao walimshambulia Mbowe kwa maneno ikiwa ni pamoja na kusema ‘tunamtaka Magufuli.”

Polisi waliokuwepo eneo la tukio, waliomba msaada na baadaye polisi wengine waliongezwa ili kukabili uvamizi wa vijana hao kwenye mkutano huo. Hata hivyo, polisi hawakukamata mtu hata mmoja licha ya kuonekana waziwazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!