Tuesday , 5 December 2023
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe avamiwa

Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, yupo kwenye wakati mgumu jimboni kwake Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea).

Akiwa kwenye mkutano jana tarehe 3 Machi 2020, alivamiwa na vijana walioandaliwa kuvuruga mkutano wake, ikiwa ni hatua za kuzima kile kilichoitwa dhamira ya kugombea tena ubunge kwenye jimbo hilo.

Mkutano huo ulikuwa ukifanyika katika Kijiji cha Kikafu Chini, Kata ya Weruweru, ambapo kikundi cha vijana wa kike na kiume liliibuka na kuanza kufanya vurugu.

Akiwa jukwaani anahutubia, ziliibuka kelele za vijana hao na kusababisha kunyamaza kwa muda, vijana hao walimshambulia Mbowe kwa maneno ikiwa ni pamoja na kusema ‘tunamtaka Magufuli.”

Polisi waliokuwepo eneo la tukio, waliomba msaada na baadaye polisi wengine waliongezwa ili kukabili uvamizi wa vijana hao kwenye mkutano huo. Hata hivyo, polisi hawakukamata mtu hata mmoja licha ya kuonekana waziwazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!